Translate

Tuesday, September 14, 2010

MBINU ZINAZOTUMIKA NA WAISLAMU ILI KUHARIBU IMANI YA KIKRISTO KATIKA KARNE YA 20-21 (21st CENTURY ISLAMIC STRATERGIES TO ELIMINATE/CORRUPT CHRISTIANITY IN AFRICA)

Utangulizi:
Leo hii, ukitembea sehemu mbalimbali hapa duniani utakutana na waislamu wengi. Waislamu wameenea kila Bara kama vile Ulaya, Afrika, Asia, na America. Inaaminika kuwa kwa kila watu watano hapa duniani, mmoja kati yao ni mwislamu. Tunashuhudia baadhi ya wakristo wakiacha imani yao na kukumbatia uislamu. Katika Bara la Afrika, uislamu umeenea kwa kasi ya ajabu. Je, ni nini kinachofanya uislamu uenee hivyo? Je, ni mbinu gani zinazotumika ili kueneza uislamu? Fuatilia somo hili ili uweze kujua hayo yote.

1. Maana ya neno "lslam"
Neno 'Islam' Asili yake ni lugha ya 'kiarabu' lenye maana ya 'utii' au 'amani'.

2. Mwanzo wa Dini ya Kiislamu
Neno "Islam" ni tofauti na "Dini ya Kiislamu". Hii ni kwa sababu neno "Islam" lilitumika na waarabu hata kabla ya kuanza kwa dini ya kiislamu. Kwa hivyo "Dini ya kiislamu", maana yake ni "kujisalimisha chini ya amri za Allah" au "Amani chini ya sheria za Allah".

i. Muhammad aliambiwa na Allah asema: -
Quran 39: 12 Suratul Zumar (Makundi / Vikosi)
"Na pia nimeamrishwa niwe wa kwanza wa (viumbe) wanaojisalimisha (kwa mwenyezi Mungu)"

Quran 6: 14 Suratul Al- An'am (Wanyama)
Sema "je nifanye mola (wangu) asiyekuwa Mwenyezi Mungu, (Ambaye ndiye) muumba wa mbingu na ardhi" naye hulisha wala halishwi" sema hakika mimi nimeamrishwa niwe wa kwanza katika wenye kusilimu na (nikaambiwa). usiwe miongoni mwa wanaomshirikisha (Mwenyezi Mungu).

Katika ufafanuzi wa aya ya 19-20, katika Suratul Yusuf 12:20 kuna maneno haya--
Unaona kuuzana kulikuwako zaidi ya miaka 4000 kabla ya kuja dini ya kiislamu aliyokuja nayo nabii Muhammad. Kisha wakausingizia uislamu kuwa ndio uliokuja na kuuza watu.

Kadiri ya aya hizi zote tunaona ya kuwa dini ya kiislamu ilianzishwa rasmi hapa duniani Ramadhan siku ya Jumatatu mwezi 17 sawasawa na Tarehe 27 December mwaka 610 Baada ya Kristo (B.K), na mtu aitwae Muhammad Bin Abdalah Bin Abd-Muttalib Bin Hashim Bin Abd Manafu Bin Kusay. Mama yake aliitwa Amina Bint Wahab.
Ama baada ya kuona mwanzo wa Dini ya uislamu sasa tuanze kuangalia mbinu za waislamu.

3. Mbinu Zinazotumika na Waislamu
Mwanzoni Muhammad, mtume wa waislamu, alitumia mbinu hata za kivita ili kueneza dini yake ya kiislamu. Hata wafuasi wake waliamrishwa kupigana kwa ajili ya dini yao. Qurani inasimulia hivi---

Qurani 5:35 Suratul Al -Maidah (Meza)
Enyi mlioamini mcheni mwenyezi Mungu na tafuteni njia ya kumfikilia (kufikilia pepo yake). Na piganeni kwa ajili ya Dini yake ili mpate kufaulu.
Katika Qurani, kitabu kinachowaongoza waislamu, zipo aya nyingi zinazowaamrisha waislamu
wapigane. Baadhi ya aya hizo ni Qurani 47:4 Suratul Muhammad na Qurani 9:123 Suratul At - Tawba. Muhammad mwenyewe alisema hivi katika kitabu cha hadithi zinazoaminiwa na waislamu wote:-

Sahih Al-Bukhari Vol. 4 Hadith na 196, Ukurasa wa 124:
Imesimuliwa na Abu- Huraira: Mtume wa Allah akasema, Nimeamrishwa kupigana na watu hadi watakaposema hakuna apasaye kuabudiwa ila Allah; Na yule atakayesema kwamba hakuna apasaye kuabudiwa ila Allah, maisha yake na mali yake yataokolewa nami…

Tafsiri ya Kiingereza:
Narreted Abu-Huraira Allah's Apostle said, I have been orderedt fight with the people till they say, none has the right to be worshipped but Allah ; his life and property will be saved by me…

Hivi ndivyo alivyosema mtume wa waislamu Muhammad,aliye mfano mwema wa waislamu wote (Qurani 33:21 Suratul Al-Ahzab). Muislamu ni lazima atekeleze kama alivyoamurishwa Muhammad na Allah. Tena tunajua kwamba, watu wote hawawezi kusema "hakuna apasaye kuubudiwa ila Allah". Hao wasiosema hivyo, kadiri ya Hadith hii, wanatakiwa kupingwa na kuawawa mara moja. Kadiri ya Qurani, miongoni mwa watu wanaotakiwa kuangamizwa ni "Wayahudi na Wakristo" (Qurani 9:30 sSuratul At-tawba). Katika kufanikisha uendelezaji wa uislamu hivi sasa, waislamu wamebuni na kutumia mbinu mbalimbali.

I. Kuunda Jumuiya na Taasisi Mbalimbali za Waislamu
Hatua ya kwanza iliyotumika na waislamu ni kuunda jumuiya. Waislamu wana jumuiya nyingi hivi sasa na taasisi nyingi Lakini nitazieleza baadhi yake.

i.Jumuiya ya Organization of Islamic Conference (O. I. C.)
Jumuiya hiyo ilianzishwa baada ya kumalizika vita kati ya Israeli na mataifa kumi na tatu (13) ya kiarabu. Vita hivyo vilipiganwa kwa siku sita na vikamalizika tarehe 5/6/1967. Katika vita hivyo waisraeli waliyashinda mataifa yote 13 ya kiarabu. Ina aminika kuwa wakati huo waisraeli walikuwa ni watu wachache wapata watu 400,000 tu. Baada ya kushindwa huko ndipo mataifa hayo 13 ya kiarabu yakafanya kikao cha kutathimini vita hivyo. Mkutano huo ulifanyika mjini Rabat nchini Morocco chini ya mfalme Hassani. Kikao hicho kilifanyika tarehe 25/9/1969 (kalenda ya kiislamu ni mwezi 12 Rajabu 1389), ndipo mataifa hayo yakaanzisha rasmi jumuiya hiyo ya Organization of Islamic Conference (O.I.C.). Hadi kufikia mwaka wa 2001, jumuiya hiyo imeweza kuwa na wanachama mataifa 56 duniani. Na juhudi zinafanyika ili kupata wanachama zaidi. Jumuiya hiyo ndiyo inayopanga na kutekeleza mbinu ya kuendeleza uislamu duniani.

ii.Kuanzisha kwa Jumuiya ya Islam in Africa Organization (I. A. O.)
Jumuiya hii ya 'Islam in Africa Organization' ilianzishwa chini ya O. I. C. na wawakilishi wa dini ya kiislamu kutoka mataifa 24 walikutana na kuunda jumuiya hiyo. Mkutano uliounda jumuiya hiyo ulifunguliwa na aliyekuwa Raisi wa Nigeria aliyeitwa Ibrahim Babangida.
Jumuiya hiyo ndiyo inayohusika kupanga na kutekeleza namna ya kuendeleza uislamu katika bara la Afrika. Jumuiya hiyo ilianzishwa tarehe 28/11/1989 kule Abuja Nigeria chini ya usimamizi wa O.I.C.

iii.Taasisi za Fedha (Tafakari kuhusu Sharia Banking System)
Ili kuendeleza dini ya kiislamu, mataifa ya kiarabu ambayo yana utajiri mkubwa unaotokana na mafuta yamezipatia nchi hizo mtaji. Utajiri wao unatumika kueneza uislamu kwa kuishambulia imani yetu wakristo kwa njia ya maneno, maandishi na Jihad (Vita Vitakatifu). Taasisi za fedha zilizoundwa chini ya jumuiya ya O.I.C. na I.A.O. ni hizi: -
Islamic Development Bank
Islamic Development Fund
Jukumu la taasisi hizo za fedha ni kuhakikisha kuwa wanatoa fedha za kuendeleza shughuli za kukuza na kusaidia nchi wanachama katika kuendeleza miradi ya uchumi, viwanda, biashara, hospitali, visima vya maji, barabara na mashule. Vile vile, taasisi hizo zinatoa fedha ili kuwashawishi hata viongozi wa mataifa mbalimbali ili wajiunge na jumuiya za O. I. C. na I. A. O. Kwa mfano, taifa ambalo lilipewa fedha nyingi mara baada ya kujiunga na jumuiya hizo za kiislamu ni Nigeria ambayo ilipewa dola za kimerikani US $ 21 BILLION. Kwa ajili ya maendeleo ya waislamu. Hata aliyekuwa Raisi wa nchi hiyo, Ibrahimu Babangida, alipokubali nchi yake iwe mwanachama wa O. I. C. na I. A. O., November 1989 kule Abuja Nigeria, Account yake iliyokuwa katika Bank inayoitwa Arab-African lnternational Bank, ilionyesha alikuwa na dola za kimarekani US $ 57.48 Billion. Aidha mawaziri wawili na mkuu wa jeshi, Account zao zilikuwa na fedha nyingi nazo zilionyesha fedha hizi:-
Mmoja alikuwa na US $ 15.2 Billion
Mwingine alikuwa na US $ 17.8 Billion
Mwingine account yake ilikuwa na US $ 24.9 Billion.
Katika moja ya machapisho yao yaliyotolewa hapa Tanzania kuhusiana na utaratibu wa fedha katika benki hizo za Kiislamu, wanasema, "chumo haram linaweza kutoharishwa na kisha kutumika kwa matumizi halali."
Chumo haram linaweza kuwa biashara haramu ya madawa ya kulevya n.k
Sheikh Yusuf al Qaradhawi wa Muslim Brotherhood, kundi la kigaidi Misri, kuhusu kupata fedha za aina hiyo kupitia Benki za Kiislamu, anasema, "kukusanya fedha kwa ajili ya mujahidina (wapiganaji wa Jihad) halikuwa suala la mchango tu au zawadi, bali ni jambo la lazima linalopaswa kufanyiwa wale wanaojitoa kwa ajili ya Vita Vitakatifu kwa ajili ya Taifa la Kiislamu."
Na hii ilikuwa ni motisha kwao. Jambo hili linatishia kuangamizwa kwa imani yetu sisi wakristo.

II. Uandishi wa Vitabu
 Waislamu wa sehemu mbalimbali hapa duniani wameandika vitabu na bado wangali wanaendelea kuandika. Vitabu ambavyo vinaisema vibaya imani yetu wakristo. Vitabu hivyo vimeandikwa katika lugha mbalimbali Kama kiingereza, Kiswahili na lugha nyinginezo. Baadhi ya waandishi wanaojulikana sana ni hawa: -

Sayyid Abul A’la Maududi
Mtu huyu alikuwa mwandishi maarufu wa kiislamu aliyekuwa anaishi bara Hindi kati ya mwaka 1903 na 1979. Aliandika kitabu kinachoitwa "Katika Kuufahamu Uislamu", mwaka 1932. Kinasambazwa na 'The Islamic Foundation', Nairobi, Kenya. Kitabu hiki kimechapishwa upya mwaka wa 1974, kina kurasa 136. Kupitia kitabu hicho, Maududi anasema katika ukurasa wa 84 kuwa "vitabu vitakatifu vya awali (Torati, Zaburi, Manabii na Injili) viliteremshwa katika lugha zilizokufa zamani". Anaendelea kusema kuwa "Hakuna nchi wala jamii inayozungumza lugha hizo sasa na ni watu wachache wanaodai kuwa wanazifahamu.
Vitabu vyake vingi vinahamasisha ushiriki katika Jihad, Vita Vitakatifu vya Kuanzisha Taifa la Kiislamu.

Pia Sayyid Abul A’la Mawdudi, katika kitabu chake kingine kiitwacho, “Jihadi katika Uislamu” kilichofasiriwa na Hassan Athman Mnjeja, katika Uk.11-13 akielezea malengo ya Utawala wa dola ya Kiislamu,  anasema: “Uhakika wa mambo ni kuwa Uislamu ni itikadi ya kimapinduzi na utaratibu unaokusudia kubadili mfumo wa jamii wa ulimwengu mzima na kuujenga upya ili ilingane na Imani na Itikadi zake. Waislamu ni jina la kile chama cha Kimapinduzi cha kimataifa chenymipango ya kimapinduzi. Uislamu unakusudia kuangamiza mataifa na Serikali zote hapa ulimwenguni ambazo ni dhidi ya itikadi na utaratibu wUislamu, bila kujal zinatawaliwa na nani. Lengo la Uislamu ni kuanzisha taifa kwa misingi ya itikadi yake na utaratibu bila kujali ni nchi gani itakuwa mstari wa mbele kusimamisha Uislamu au ni utawala wa taifa lipi

utahujumu mpango wa kuanzisha taifa la Kiislamu ……kubadili mifumo ya zamani ya kidhalimu na kujenga mfumo mpya wenye haki na usawa kwa kutumia upanga, ni Jihad vilevile.”

 Ahmed Deedat
Mtu huyo Deedat ndiye mwandishi maarufu wa vitabu. Ahmed Deedat anaishi kule Durban, Afrika Kusini. Shirika lao linaitwa 'The Islamic Propagation Centre'. Ukisoma vitabu vyake utaona jinsi anavyotumia hisia zake kutoa tafsiri potofu kupotosha maandiko matakatifu ya Biblia. Deedat ndiyo chanzo kikubwa cha mihadhara iliyoenea sana duniani na hasa katika nchi za Afrika Mashariki na Kati. Vitabu vyake pia vinatumika katika Makongamano, Semina, Mihadhara na kwenye Website mbalimbali. Waendesha mihadhara wamechukua hoja zipatazo 150 alizoziandika. Katika kitabu chake kinachoitwa "The God That Never Was" (Mungu Asiyekuwepo Kamwe), chenye kurasa 15 alichokiandika mwaka wa 1983, Deedat anasema hivi, "Kusema kwamba Yesu ni Mungu siyo tu kudhihaki Mungu, bali ni kukufuru kwa aina mbovu kabisa na ni kutukana hata akili ya mwanadamu". Anaendelea kusema "Yesu ni Mungu mlafi na mlevi" (Mathayo 11:19), "Mungu ambaye hakujua kusoma na kuandika" (Yohana 7:14-15), "Mungu aliyekuwa wa kabila la wayahudi" (Ufunuo 5:5), "Mungu aliyezidiwa na hisia zake" (Marko 14:33), na "Mungu bubu na asiyejikinga" (Matendo 8:32). Ukisoma kitabu hiki utasikitishwa sana na lugha mbaya za Deedat ambazo waislamu wanazishangilia na kuzitumia katika mihadhara yao. Isitoshe jumuiya kubwa za O.I.C., Islamic Development Bank na Mfalme Fahad wa Saudi Arabia ndio wafadhili wake wanaomsaidia kusambaza vitabu hivi duniani kote. Hii ni hatari kwa imani yetu sisi wakristo.

Prof, M. H. Maliki
Profesa Maliki ndiye mshauri wa wanafunzi waislamu katika chuo kikuu cha Nairobi. Ameandika kitabu kinachoitwa "The Mission of Jesus" (Ujumbe wa Yesu). Amekiandika mwaka wa 1993, kina kurasa 117 na kinaenezwa na "Islamic Foundation" Nairobi, Kenya. Katika kitabu chake anasema maneno mabaya ya kuvuruga wakristo. Naye anasema hivi: -
Yesu amemtabili Muhammad
Vitabu vya injili haviaminiki
Injili ya barnaba ni injili halisi
Paulo alibadili injili ya Yesu
Kumkubali Paulo ni kumkataa Yesu
Isitoshe profesa Maliki ameandika mara nyingi katika gazeti maarufu la kiislamu linaloitwa 'Al-Islam' kwa miaka mingi.

Ali Muhsin
Ali Muhsin ni mtu maarufu ambaye zamani alikuwa waziri katika nchi ya Zanzibar. Na alifungwa jela miaka kumi 10 Kitabu alichoandika kinaitwa "Let the Bible Speak" (Acha Biblia Ihukumu), chenye kurasa.169 Kimechapishwa na Ansaar Muslim Youth Organization, Mombasa, Kenya. Katika kitabu chake, Muhsin anasema hivi…
Yesu alikuwa Nabii mwema wa uislamu lakini alikufa kabla hajakamilisha utume wake, maisha yake mafupi yalimzuia kukamilisha utume ambao alitumwa aulete duniani.
Mwanzilishi wa ukristo ni Paulo
Paulo ni mtu mbaya aliyeingiza imani ya dhambi ya asili, wokovu kwa njia ya damu. Na fumbo lisilo eleweka kabisa la utatu.
Muhsin anaendelea kusema kuwa, mafundisho ya Paulo yamewachanganya wafuasi wa Yesu na kuwazuia wasimkubali Muhammad.

Sheikh Muzaffar Ahmad Durani
Vitabu alivyoandika ni vingi. Hapa ninavitaja viwili tu :-
Silaha za mahubiri
Zawadi kwa wakristo
Waenezaji wa vitabu hivyo ni jumuiya ya waislamu wa Ahmadiyya. Yaliyomo katika kitabu cha zawadi kwa wakristo ni haya:
Ukurasa wa 21 Yesu si Mungu kwa sababu alioa
" 22 Mke wa Yesu Mariam Magdalena
" 28 Yesu alitumwa kwa wana wa waisraeli tu (Mathayo 15:24)
" 31 Yesu aliteta upanga (Mathayo 10:34-35)
" 39 Paulo ni mhalifu wa Yesu( Matendo 26:9)
" 43 Bwana Yesu hakufia msalabani (Waebrania 5:7)
" 96 Nyimbo hazitakiwi (Amosi 5:23)
Nchini Kenya, jumuiya ya Ahamadiyya Muslim Mission imetafsiri Qurani katika Lugha za Kiswahili, na pia wametafsiri Qurani ya Kikuyu iliyotafsiriwa mwaka wa 1988, pia wana mpango wa kutafsiri Qurani kwa lugha za Kikamba na Kijaluo. Je mkristo, vitabu hivi vinaashiria nini kwako? Vinalenga kuharibu imani yetu au la? Tafakari.
Dar-es-Salaam, Tanzania Waislamu walikuwa na njama ya kuchapisha Biblia potofu, milioni 15, ambazo zingeonyesha utabili wa Muhammad. Angalizo kuna injili ya upotofu iitwayo "Injili ya Barnaba".

III. Vijarida (Tracts)
Waislamu wanachapisha vijarida na kugawa. Vingine vinawekwa hata mashuleni ili visomwe. Kijarida kimoja kilichoandikwa chasema "Yesu hakuzaliwa Tarehe 25 December".

IV Vikundi vya mihadhara.
Vikundi hivyo ni vingi na vimeenea sana katika za Afrika Mashariki na kati, na hadi kufikia mwaka 2001 kulikuwa na vikundi 15. Vikundi hivyo vinatumia Biblia Takatifu na wanatoa mafundisho potofu.

V. Magazeti (Newspaper)
Yapo magazeti mengi yanayoandika habari za kupotosha maandiko matakatifu ya kweli ya Biblia. Baadhi ya magazeti yameingizwa katika 'Internet' na 'Website' -
i. Magazeti yanayochapishwa nchini Tanzania:
An – Nuur.
Nasaha. 
Mapenzi ya Mungu.
ii. Magazeti yanayochapishwa nchini Kenya:
Al – Islam.
International Bulletin
Al-Madrasah
Sauti ya Umma
The Guide
Dunia-e-Farsi

VI. Internet na Website
Mafundisho ya kupotosha Biblia na hoja potofu zilizotengenezwa na waislamu dhidi ya wakristo siku hizi yanaonekana sana katika intenet na website nyingi Baadhi yake ni hizi: -
AI. Haramain Foundation (www. Alharamain .org )
Islam 101 (http://www.islam101.com/)
Al. Huda/the qur’an .com
The shia home page (http://www.shia.org/)
Jambo la kushangaza unaloweza kukutana nalo katika websites zao ni kuwa Qur’an iko sawa, haina makosa kwa asilimia 100. Lakini wanasema kuwa Biblia ina makosa 50,000.

VII. Kanda za Audio na Video (Cassettes)
Hizi ziko nyingi tu katika kanda mojawapo Ahmed Deedat anasema kwa kusisitiza kuwa katika Biblia hakuna injili wala Torati, bali iliyokuwepo ni injili kama, yaani "The Gospel according to Matthew, Mark, Luke and John".
Vile vile waendesha mihadhara wanarekodi kanda nyingi za video na audio na kuzisambaza sehemu mbalimbali duniani. Kwa mfano, nchini Kenya, kanda hizo zinasambazwa na Iranian Cultural Centre.

VIII. Ujenzi wa Misikiti (Building of Mosques)
Miongoni mwa mbinu zinazotumika kueneza uislamu ni ujenzi wa misikiti mizuri na mikubwa. Katika misikiti hiyo vimewekwa vipaza sauti (loud speaker) ambavyo vinatoa sauti kubwa sana. Wapiga adhana huanza kuwahamasisha watu waende kuswali (kusali) kuanzia saa kumi alfajiri (4:00 A.M.). Wapiga adhana hao wanatumia maneno makali ya kuwatisha watu wanaposema "hicho kitanda chako ni jeneza, chumba chako ni kaburi na shuka lako ni sanda". Misikiti mingine hujengwa kwenye maeneo ya umma (public areas) kama vile maofisini, viwanjani ambavyo si maeneo rasmi ya dini ya Kiislamu (majina na maeneo ilipo misikiti hiyo imehifadhiwa)
Ujenzi wa misikiti hivi sasa unazidi kuenea kwa kasi ya ajabu baadhi ya nchi ni hizi --

Uingereza, Ujerumani na Ufaransa - kila baada ya wiki mbili msikiti mmoja mpya unafunguliwa.
Ethiopia – wakati wa utawala wa kikomusti nchini humo kwa miaka mitano (5) tu, misikiti 5002 ilijengwa
Malawi – kila umbali wa kilometa (15) msikiti mmoja umejengwa
Botswana – miaka kadhaa iliyopita walikuwepo waislamu wachache sana. Lakini hivi sasa, nchini humo imejengwa misikiti mingi.
Tanzania – nchini humo ukitembelea katika mji wa Dar-es-salaam utaona kuna misikiti mingi mikubwa na gharama kubwa ukienda katika barabara ya Iringa na Mbeya utaona kuwa kwa kila kilometa 10, msikiti mmoja umejengwa.
Siera leone - ijapokuwa nchi hiyo ndiyo ya kwanza kufikiwa na Injili kati ya mataifa ya Afrika magharibi yapata miaka 200 iliyopita. Lakini kwa sasa, idadi ya wakristo haipiti asilimia kumi. Nchi hiyo ina Misikiti ipasayo 3,812 na idadi ya waislamu kwa sasa ni asilimia 40. Watu wa makabila ya Yalunka, Temne, Mende, Koranko na Loko wanasilimu na kujiunga na uislamu kwa wingi sana.

IX. Ndoa (Marriage)
Hii ni mojawapo ya njia inayotumika katika kuendeleza uislamu kwani Qur’an inawaagiza waislamu waoe wake wengi, nayo inasimulia hivi--
Qurani 4:3 Suratul An Nisaa (wanawake)
Na kama mkiogopa kutowafanyia uadilifu mayatima (basi ogopeni vilevile kutowafanyia uadilifu wanawake). Basi oeni mnaowapenda katika wanawake, (maadamu mtawafanyia insafu) wawili au watatu au wanne (tu)…
Aidha Qur’an inatoa ruhusa ya kubadili mke kwa kumuacha mke wa zamani na kuoa mwingine (Surah 4:20) waislamu hufanya bidii ya kuwatafuta wasichana wakristo na kuwabadilisha dini na kuwaoa. Hivyo kusababisha kuongezeka haraka. Ili kuhakikisha idadi yao inaongezeka waislamu pia wameunda vikundi vya wanawake, kwa mfano Tanzania kuna vikundi viwili ambavyo wanasaidiwa kifedha ili kuwatafuta wasichana wakristo hata vijijini katika mikoa mbalimbali kwa kisingizio cha kuwapatia kazi za house girl kisha wanawasilimisha na kuwaozesha.
Vikundi hivyo ni hivi: -
Saraffiya women Development Islamic Group
Al-Mubaraghat Islamic Group
Nchini Kenya kuna kikundi cha wanawake kinachoitwa "Ahli- Sunat Women Group". Je wakristo, tunafanya juhudi gani kuwafikishia injili watu wasio wakristo?

X. Ajira (Employment)
Kupitia jumuiya ya kiislamu ya O.I.C. na I.A.O. pamoja na Taasi za fedha za Islamic Development Fund, Islamic Development Bank na African Muslim Agency, fedha nyingi zinatolewa kufungua miradi mbalimbali ya uchumi, biashara na viwanda. Kwani O.I.C. inatoa mikopo na kujenga viwanda katika nchi mbalimbali. Wafanya biashara wakubwa wa kiislamu hupewa fedha za kufungua viwanda ambapo wanawashawishi watu kwa vigezo vya kuajiriwa na hatimae wanawasilimisha.
Baadhi ya viwanda vinavyomilikiwa na waislamu nchini Tanzania wamejenga misikiti ndani yake, na hata katika vituo vya kuuza mafuta (Petrol Station) kuna misikiti. Je, ni wakristo wangapi wanajenga makanisa katika viwanda?. Maajenti wa O.I.C. ina aminika wapo hata katika kiwanda kimoja cha kutengeneza sukari, ambacho kinamiliki timu ya mpira. Kupitia maajenti hao hivi sasa tayari mchezaji mmoja, mlinda mlango(goal keeper) na kocha mmoja (asiye raia wa Tanzania) wamesilimishwa ili wawe na ajira bora. Nchini Uganda, Chuo Kikuu cha Kiislamu kinawavutia wasomi wengi, hata maprofesa wakristo, kwa sababu kinatoa mishahara minono.

XI. Elimu (Education)
Nchini Botswana ambapo miaka kadhaa iliyopita walikuwepo waislamu wachache hivi sasa shule nyingi zimejengwa zikiambatana na misikiti wanafunzi hupata elimu bure hadi kiwango cha shahada (Degree). Na wakati mwingine masomo katika nchi za ng’ambo katika vyuo vikuu vya kiislamu.
Nchini Uganda chuo kikuu cha kiislamu kinawavutia sana wanafunzi wakristo kwani waweza kupatiwa masomo bila malipo.
Nchini Tanzania pale Dar-es-salaam kuna shule moja inadhaminiwa na Kuwait masomo kwa waislamu kuanzia primary hadi secondary ni bure. Isitoshe waislamu kabla ya uhuru na baada ya uhuru hadi kufikia mwaka wa1990 walikuwa chini kielimu kwa asilimia 10. Lakini kuanzia mwaka wa 1991-2001, waislamu wamepanda kielimu na kufikia asilimia 48. Hivi sasa wanaendelea kujenga shule zaidi.
Nchini Kenya, mashirika ya Iranian Cultural Centre, Al-Rasul Al-Akram Islamic Centre, Islamic Foundation na International Islamic Relief Organization of Saudi Arabia wanafadhili miradi ya shule na madrassa. Pia, mashirika hayo yanafadhili wale wanaotaka kujiendeleza zaidi kielimu.
Vilevile nchini Kenya shirika la African Muislim Agency wamejenga chuo kiuu cha kiislamu kipo huko Thika na kilifunguliwa mwaka wa 1978. kila mwanafuzi anapata elimu bure kwa miaka minne, na kinafadhiliwa na nchi za Kuwait na Saudi Arabia.Kkazi kubwa za taasisi hizo za kidini ni "kusilimisha ufahamu wa wanafunzi" Je, wakristo tunafanya nini?

XII. Afya (Health)
Shirika la maendeleo la waislamu liitwalo African Muslim Argency limefungua hospitali mbalimbali, na kupitia hospitali hizo utashangazwa kuona gharama ya matibabu inaweza kuwa kubwa kwa mkristo, na ikawa ni ndogo kwa mwislamu. Wahudumu wa hospitali hizo wanawashawishi wakristo ili wasilimu ili wawasaidie kwa matibabu mazuri. Nchini Kenya, shirika la International Islamic Relief Organization of Saudi Arabia limefadhili miradi ya ujenzi wa vituo vya matibabu (Dispensaries) katika miji ya Mombasa, Machakos, Wajir na Elwak. Hii ni hatari kwako mkristo kuacha imani yako.

XIII. Visima vya Maji
Visima hivi vimejengwa kwa wingi na African Muslim Agency katika mji wa Dar-es-salaam. Misikiti mingi ina visima vya maji ambavyo vinatumika. Pia vinawavutia baadhi ya wakristo kwa sababu ukitaka maji katika visima hivyo ni lazima usalimie "Asalam aleykum". Nchini Kenya, shirika la International Islamic Relief Organization of Saudi Arabia limefadhili miradi ya kuchimba visima vya maji sehemu kame. .Je, hilo linaashiria nini kwako mkristo?

XIV. Vituo vya Watoto Yatima (Centre for Orphans)
Nchini Kenya, mashirika ya Iranian Cultural Centre, Al-Rasul Al-Akram Islamic Centre, Islamic Foundation na International Islamic Relief Organization of Saudi Arabia yanafadhili vituo vya watoto yatima.Tanzania pia kuna vituo vya aina hiyo kule Mwanza na Rukwa.  Vituo hivyo vya kulelea watoto yatima vinawasilimisha wale ambao ni wakristo. Vile vile, wale wanaowalea wanasilimishwa ili wasaidiwe.  Watoto waliosilimishwa katika vituo hivyo, na wale waliokuwa Waislamu tangu kuzaliwa wanaolelewa kwenye vituo hivyo, kwa pamoja, huanza kufundishwa mafunzo maalumu yanayoitwa "kuusilimisha ufahamu. "Je, kumsaidia mtu ni lazima awe wa imani yako?

XV. Uchawi na Ushirikana (Witchcraft and Sorcery)
Waganga wakienyeji ambao wengi ni waislamu wanawashawishi wagonjwa wakristo wasilimu kwa madai kuwa ili matibabu yafanye kazi. Basi jina la kikristo libadilishwe na upewe jina la kiislamu, ndipo matibabu yatafanikiwa. Tahadhari kwa wakristo wenye tabia za kwenda kwa waganga wa kienyeji.

XVI. Vituo vya Radio na Televisheni (Radio Station and Television)
Njia nyingine inayotumika kueneza uislamu ni vituo vya radio na televisheni ambavyo waislamu wamevijenga. Kwa mfano, Televisheni ya Al-jazira mara kadhaa inatoa matangazo ya kuonyesha kuwa wakristo wa nchi za magharibi ni maadui wa uislamu. Nchini Kenya, ipo Radio Station itwayo IQRA F.M. 95.1. Wanaendesha kipindi kinachoitwa "Dini ya Haki". Wanatoa mafundisho potofu kwa kusema, "Yesu hakufa msalabani", "Paulo si mtume wa Mungu", "Ukristo siyo dini", na "Yesu sio Mungu". Pia huko Mashariki ya Kati imejengwa stesheni ya redio ambayo ina nguvu kubwa ya kupeleka matangazo. Redio hiyo ina 'transmitters' zenye nguvu za 2000 K.W., wakati stesheni ya redio kubwa ya wakristo ya kueneza injili ina 'transmitters' zenye nguvu ya 50 K.W. Wakristo tuwe makini na utangazaji wa injili tukikumbuka kuwa lnjili ndiyo uweza wa Mungu unaoleta wokovu (Warumi 1:16; na Marko 16:15-16). Isitoshe lnjili ndilo neno pekee la kweli ya Mungu (Wakolosai 1:15).

XVII. Misaada ya Vyakula
Shirika linaloitwa Ahmadiyya Muslim Mission linatoa misaada ya vyakula ili kuwavutia watu wasilimu na kuwa waislamu.

4. Idadi ya Waislamu
Ongezeko la waislamu duniani linatisha sana, kwani miaka mia moja 100 iliyopita, yaani 1900, waislamu dunia nzima walikuwa 14 Million. Lakini idadi ya waislamu imeongezeka kwa kasi ya ajabu, kwani hadi kufikia mwaka wa 2000, waislamu duniani kote wamefika 1.5 Billion. Ongezeko hilo la waislamu ni kubwa sana ukilinganisha na ongezeko letu wakristo. Kwani wakristo duniani kote miaka 100 iliyopita walikuwa 558 Million na hadi kufika mwaka wa 2000 wakristo duniani kote tumefikia 2.1 Billion tu. Katika Bara la Afrika peke yake, kuna idadi ya waislamu ni 324 Million. Yafuatayo ni baadhi ya mataifa yenye waislamu wengi:-


Bara la Afrika
Nchi Waislamu Asilimia(%) Wakristo Asilimia (%)
Tanzania 13 Million 40 17,234,449 51.42
Kenya 3.3 Million 10 23,655,205 78.64
Uganda 2.0 Million 7 19,306,596 88.65
Moroco 28,178,512 99.85 28,221 0.10
Libya 5,408,557 86.52 168,142 3.00
Misri 59,239,980 86.52 8,887,366 12.98
Nigeria 45,717,499 41.00 58,663,357 52.61

Bara la Asia
Nchi Waislamu Asilimia (%) Wakristo Asilimia (%)
Bangladesh 110,556,810 85.63 929,917 0.72
India 126,707,722 12.50 25 Million 2.40
Pakistan 150,349,015 96.08 3,614,761 2.31
Indonesia 171,032,517 80.30 34,078,708 16.00
Saudi Arabia 20,057,491 92.83 980,944 4.54

Bara la Ulaya
Nchi Waislamu Asilimia (%) Wakristo Asilimia (%)
U/ Kingdom 1,176,603 2.00 39,786,837 67.63
Ufaransa 5,907,971 10.00 40,008,779 67.72



KUHUSU TANZANIA:  Abd Al-Masih katika kitabu chake Holy War in Islam, uk. 55-56
akielezea kuhusu hatua mbali mbali za mapambano ya jihad katika Uislamu (Radicalization Process)anasema:- "Katika nchi ambazo wakazi wake wengi ni Waislamu, lakini ambako
Taifa la Kiislamu bado halijaanzishwa, matengenezo ya Uislamu, yanaweza
kutokea, yakilenga kungo’a mabaki yote ya Ukristo, pamoja na ukoloni
wa kimagharibi katika nchi husika. Kwa hakika kunakuwa na nguvu kwa
ajili ya kuondosha tawala zilizopo ili kusimika utawala ule unaoweza
kutekeleza sharia. Katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Sudan, Waislamu
wengi wanadai kwamba sharia zinapaswa kurejeshwa tena na kuwa ndizo
pekee ziwe mfumo rasmi wa taratibu za sheria ya nchi.
Lebanoni, Malaysia, Nigeria na TANZANIA, ni mifano ya kuonesha
migongano ya majaribio ya muda mrefu yenye kuhusisha uanzishwaji wa
Taifa la Kiislamu. Wakazi wake wengi katika nchi hizo si Waislamu. Licha ya uwiano huu,
viongozi ambao ni Wakristo huondolewa mmoja mmoja kutoka kwenye
vyeo vyao vyenye ushawishi, na magazeti na vyombo vingine vya habari,
hukithirisha kutangaza propaganda za Uislamu. Mazingira katika nchi hizi, mara kwa mara huwa ni yenye kujawa na wasiwasi na yenye jazba. "

Haya ni mambo ya kutafakari. Tukumbuke kuwa Bwana Yesu alianzisha kanisa miaka 577 kabla ya Muhammad hajaanzisha Dini ya Kiislamu. Yatufaa tujue kupigwa vita huku kwa ajili ya imani yetu na nchi zetu. Lazima tuamke sasa. Wakati wa kulala umepita. Tutumie wakati wetu wote tukiongozwa na Roho Mtakatifu ili tuliokoe kanisa la kristo na nchi yetu. Yatupasa kuanzia katika bara letu la Afrika na baadaye dunia nzima. Watu wa bara hili la Afrika wanatakiwa kujua habari njema na wakupeleka Injili hiyo ni sisi sote.
 Yafaa kila mkristo kujiuliza swali hili akiongozwa na aya ya Warumi 8:35-36 Ni nani atakayetutenga na upendo wa kristo? Je! ni dhiki, au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, ua upanga?. Kama ilivyoandikwa ya kwamba, kwa ajili yako, tunauawa mchana kutwa, tumehesabiwa kuwa kama kondoo wa kuchinjwa. Ndugu mpendwa, natumai kwamba umezijua mbinu zinazotumiwa kueneza uislamu. Utajitahidi kuwafahamisha wengine ili wasiongozwe na elimu za uongo na tamaa ya mali na kumwacha Bwana Yesu (Waefeso 4:15).
KWA UWEZO WA MWENYEZI MUNGU, MAJIBU YOTE BIBLIA INAYO.TUNATAMANI NA SISI KUCHAPA VITABU VINGI ILI KUJIBU MASWALI YOTE NA KUWAELEKEZA WAISLAMU KWENYE MSALABA WA KRISTO ILI WAPATE WOKOVU. KANISA KAA MACHO NA MBIZU HIZI NA NYINGINE NYINGI ZA AINA HIYO ZITAKAZOJITOKEZA. MILANGO YA KUZIMU HAITALISHINDA KANISA (MATH 16:18)

47 comments:

Anonymous said...

UMEPATA WAPI TAKWIMU HIZOI ZA IDADI YA WAISLAM NA WAK|RISTO TANZANIA?.

Anonymous said...

Mara nyingi tunapokuwa tunatembea barabarani tuwe tunaenda kazini, shuleni au popote pale huwa tunakutana na Wakristo wanaotuita tuingie kwenye Ukristo, utashangaa mtu anakusimamisha anakwambia Yesu anakupenda ndio maana amenikutanisha na wewe leo, mpokee ili uokoke. Wengine wanakufuata nyumbani kwako kukuletea huo ujumbe, Hii ina maana gani? Kwanini mtu umfuate nyumbani kwake au umsimamishe barabarani umwambie aingie kwenye dini yako? HILI HUJALIONA KUWA NI TATIZO? BIASHARA ILIYOKUWA NZURI MTU ATALAZIMISHWA KUNUNUA? BIASHARA HUWA INAJIUZA YENYEWE KWA UZURI WAKE MTU AKIIONA ANAIFATA, UKIONA BIASHARA MTU ANAKULAZIMISHA KUNUNUA IJUE HAIFAI. Waambieni hao watu zenu wanaotangaza Injili kwa nguvu huko barabarani, wanatukera vile wanavyotuita CHEMA HUJIUZA KIBAYA HUJITEMBEZA.

THE VISION said...

Wewe Mwankemwa acha unafiki unahimiza wenzako mbona wewe na kundi lenu mnaojiita christian power mmeshindwa kuitetea hiyo imani yenu ya kikafiri pale Diamond Jubilee na PTA hata kupoteza baadhi ya waumini wenu mbele yako wewe na mwenzako.
Kaka njoo kwenye haki.KUMBUKA MANABII WOTE WALIKUWA WAISLAM WEWE JE NANI? AU ND'O KUNI ZENYEWE?

Anonymous said...

"ISLAM:Spritually Myth, Historically False, Mathematically Absurd!"
UMEMZUMGUMZIA SHEKH AHMED DEEDAT (MUNGU AMWEKE PEPONI INSHAALLAH) KUWA AMEUTUKANA UKIRISTU. NAAMIN UMEANDIKA HIVI KWA SABABU WEWE UNAPENDA HAKI NA SIYO DHULMA KAMA MAFUNDISHO YA KIKRISTU YALIVYO.
JE KICHWA CHA HABARI KWENYE BLOG YAKO KIMEUKASHIFU UISLAM AU KIMEUSIFIA NAOMBA JIBU.wakiristu mnazidi kuonesha chuki zenu dhidi ya dini tukufu ya Islam lkn inshaallah M/Mungu anajua hizi dhulma zenu na ataziangamiza.

vilevile wakiristo mnapotosha sana mafundisho ya dini yetu tukufu na hili umethibitisha baada ya kusema Uislam umeenea kwa sbb ya upanga hayo maneno hutakiwi kumdanganya mtu swali: UISLAM umesambaa sana ULAYA kwa kipindi cha karne 1 iliyopita na ndiyo dini inayokuwa kwa kasi kubwa nchi za Ulaya
je km kweli uislam unaenea kwa upanga ni jeshi gani la kiislam limeenda kupigana na kuwasilimisha watu kwa nguvu huko America na Ulaya? for sure hakuna KUMBE SASA NI NINI KINAFANYA WATU WANAINGIA KTK DINI KWA WINGI? NI UKWELI WA DINI YA KIISLAM NDO UNAFANYA WAZUNGU WANAKUBALI.
2. CHUKI ZA MATAIFA YENYE ITIKADI KALI ZA KIKIRISTO KAMA AMERICA (ROMAN CATH) NA EURO (ANGLICAN) NDO TUMEONA KWA WINGI WAKIZIVAMIA NCHI ZENYE ITIKADI ZA KIISLAM AU ZENYE WAISLAM WENGI ILI KUUENEZA UKIRISTU KWA UPANGA, KWA MFANO AMERICA NA MSHIRIKA WAKE ENGLAND WAMEVAMIA IRAQ, AFGHN,NA UTAWALA WA KIZEYUNI NA HARAMU WA ISRAEL KUIKALIA KIMABAVU PALESTINE NA KUWAUWA WATOTO NA WANAWAKE BILA HURUMA.
3. NCHI HIZO HIZO ZIMEIVAMIA CHECHNYA NA BOSNIA NCHI AMBAZO ULAYA ZINA WAISLAMU WENGI NA KUWAUWA MAELFU KWA MAELFU KWA SABABU TU NI WAISLAMU (CRUSADE WAR)
UKIRISTO UNATAKA KUENEA KWA NJIA YA UPANGA SASA MANAKE KWA NJIA YA AMANI IMESHINDIKANA KABISA
4.WAKIRISTU KWA ROHO MBAYA MMEKATAA OIC HAPA TANZANIA LAKINI MBONA MASHIRIKA YA KIKIRISTU YAPO MAMIA NA MAMIA KAMA PARTAGE,ICAP,KAEMP.E.T.C HUMU KOTE MUISLAMU HAPATI AJIRA HIYO MBONA HUKUISEMA NDUGU!!
5.UMEZUNGUMZIA ONGEZEKO LA MISIKITI DAR, LAKINI ONGEZEKO LA MAKANISA YASIYOKUWA NA WAUMINI HUKO ZANZIBAR MBONA HUKUYASEMA
6.MoM KAMA KWELI SERIKALI HAIRUSIWI KUINGILIA MAS-HALA YA DINI MBONA SERIKALI INACHOTA MAFEDHA ILI WAWAPE MUENDELEZE TAASISI ZENU!
7.MMEPEWA MSAMAHA WA KODI BIDHAA ZA KANISA ZINAZOTOKA NJE NA MNAFANYA BIASHARA KWA MGONGO WA DINI KUPITIA MSAMAHA! HIVI NYIE SI NDO WA KWANZA KUIKASHIFU INJILI KWA KUIWEKA KANDO NA KUTAFUTA MASLAHI YA KIDUNIA!
8.UMENUKUU SURA ZA QURAN NA KUZITAFSIRI KWA MAPENZI YAKO LAKINI HEM TUMSIKIE YESU KRISTU ANASEMAJE KTK INJIL YA LUKA 12:51 MSIDHANI YA KUWA NIMELETA AMANI DUNIANI? NAWAAMBIA LA SIVYO BALI MAFARAKANO.
MATHAYO 10:34-35 "MSIDHANI YA KUWA NIMEKUJA KULETA AMANI DUNIANI LA SIKUJA KULETA AMANI BALI UPANGA...." NDIO MAANA TUNASHUHUDIA NCHI ZENYE MSIMAMO MKALI WA KKRISTO WANATUMIA UPANGA KUVAMIA NCHI ZENYE WAISLAM WENGI ILI KUWALAZIMISHA KUKUFURU (KUWA WAKIRISTU)
9.HIVI HATA AMERICA NA ULAYA WANASILIMU ILI WAPATE AJIRA OIC?ACHA UCHOCHEZI NDUGU.
UKITAKA KUJUA KWA NINI WAISLAMU WANAONGEZEKA KWA KASI DUNIANI NENDA YOU TUBE ANDIKA NENO HILI CONVERTS TO ISLAM UTAPATA KUJUA WHY ISLAM IS A CURRENT RAPID GROWING RELIGION IN THE GLOBE.LET ME WIND UP WITH QURANIC VERSE WHICH SAYS 17:71 " Na sema: Kweli imefika, na uwongo umetoweka. Hakika uwongo lazima utoweke!"

Unknown said...

Hivi vyakuandika vimeisha au unatafuta umarufu kwa kimvuli cha dini yapo mengi ya kuandika saana tu nyie ndiyo mnaesababisha vurugu za kidini zisiishe kutokana hamna mambo ya kuandika basi tumia blogspot yako kwa manufaa ya wote kama hauna vitu vya kuandika acha we zube nini au andikeni kuhusu dini yenu basi tumia brain pia we ni msomi unaijua vema nchi kama vipi nenda kalime tu utekeleze kaulimbiu ya kilimo kwanza kuliko kuandika utumbo huu

Anonymous said...

Mkristo atakayemkana Yesu na kuwa muislamu ni wa kuombewa ana mapepo!

Unknown said...

Napenda kuanza kwa kumshukuru mungu alie mmoja hakuzaa wa hakuzaliwa.
Ukweli nime jiuliza maswali mengi kutokana na maelezo yako ikiwemo lile ulo sema kuwa " waislam wanatumia Bilblia ya upotofu ya 'Barnaba' " ilhahi ndio Biblia ambayo ina fichwa na Maaskofu kwa lengo tu lakuta kuwapoteza wakristo wasi mfuate mtume wetu Muhammad(s.w.a) ambae ni Mtume wa haki alie Tabiriwa kwa jina na mtume wa Allah ambae ni Issa(yesu)(a.s).

Anonymous said...

KHATIB.

Ndugu nikuelimishe tu njia moja kubwa zaidi ambayo hukuitaja inayosaidia kuisambaza dini takatifu ya Kiislam ni hii ya kujitia kubishana nayo au kujaribu kuitia kasoro. Ona sasa ulivyoisifia kwa kusambaza sifa zake njema za amani, umoja na upendo... Hakuna hata nukta moja inayo ashiria mabavu kinyume na ulivyotaka wakristo waamini.
Tabaan umewastaajabisha sana wakristo wenzio na kuwashtua kwa TAKWIMU za kutisha za ukuaji na ustawi wa UISLAM duniani, dhidi ya njama nyingi zenu nyinyi wakristo na Mayahudi ambazo umejaribu kuto kuzitaja ila wakristo wenyewe mnazielewa...
Mkiristo mwenye akili lazima ajiulize jee mbinu zote hizi kumbe bado muko nyuma?? Kumbe bado mumeshindwa??

Kwa nukta hii ama umewachanganya wakristo wenzako, umewachukiza ama wameuona ukweli.. Angalia wakokimyaa..! wachangiaji wote ni waislam hadi sasa... Wao Hawana la kukupongeza ila mimi nasema Heko.. Kweli maneno ya Allahu hayana makoseo 100% na kama alivyomalizia Anonymus ( " Na sema: Kweli imefika, na uwongo umetoweka. Hakika uwongo lazima utoweke!") HEKO KWA KUUENEZA UISLAM.

Anonymous said...

SONGA MBELE MTUMISHI

Anonymous said...

data zako feki na hoja zako hazina msingi kabla ya kuanza kuchambua jitahidi kusoma intensively no research no right to talk. Pia soma ukristo wako vizuri.

emmanuel !!! said...

Le bro khajk mapo kleghrtyu jkdmse jhende ksimeyt haim kshajung kipkloe gygahguwu hjsiu bgygdy dgvj p hgk twm. amen

Anonymous said...

Hapa cha kusema ni kwamba hawa wanaosilm si kwamba wameelimishwa la hasha,bali ni wapenda taama za mwili kama kuoa wake wengi na kazalika .tena wa islam hawana roho mtakatifu wanayoyazungumzia ni ya kimwili tu.wale wote waliyoandika vitabu vile na kutoa maandiko hakili zao ziko hapa yaani hawa oni mberena aliyekuja kuwakomboa hawakumjua.1peter 1:9-11;Isaya 11:1-4

Anonymous said...

Inshallah mwemyezi atusaidie kuutambua ukweli

Anonymous said...

Nakupongeza sana ndugu Daniel, kwa kusaidia kuonyesha ukweli huu. Wakristo tuache ubinafsi na umadhehebu kujifanya tu bora kushinda dhehebu jingine, tuungane sote kupambana na huyu adui yetu mkuu, maaskofu kuanza kulumbana kama kina gwajima na pengo ndiko hata kulikosababisha katika karne za mwanzo za ukristo kule Mashariki ya kati Afrika kaskazini na Ulaya ya mashariki kutekwa na hawa jamaa Waislamu, Roma na Kanisa la Orthodox kukosa umoja ndiko kulikosababisha waislamu wakatushinda vibaya wakanyakua maeneo yaliyokuwa chini ya wakristo kama Misri, Uturuki na Palestina. Mbinu walizotumia ndio hizohizo hata leo wanazitumia pamoja na Ugaidi. Wakristo tuamke tujibu Hoja moja baada ya nyingine , Wakitoa kitabu, na sisi tukijibu kwa ukubwa uleule, wakitoa mkanda wa kashfa tuujibu siyo kwa kashfa bali kwa busara ya kuonyesha uwongo walioutoa katika kanda husika. Tuzidishe na sisi machapisho, kanda, dvd vipindi vya redio na mitandao ya kompyuta kujibu uwongo huo. Halikadhalika kama Kanisa katoliki linavyohimiza watu wazae watoto wengi kadiri inavyowezekana kukabiliana na mbinu yao hii chafu ya kuoa wanawake wengi. Tujitahidi piakuinuana kiuchumi pamoja na kielimu zaidi. Badala ya kuendekeza mgawanyiko kwa kuanzisha utitiri wa vidhehebu tuboreshe yale yaliyokuwepo pamoja na kuweka mikakati ya kupambana na mbinu hizi chafu ambazo ndiyo adui namba moja sasa wa Ukristo Duniani. Tusijidanganye eti tunaishi nao kwa amani ili hali wakitumia mbinu za kila aina kututokomeza, kama hizi za ugaidi kule kenya na Nigeria. Uislamu hauna nguvu ya kusimama peke yake pasipo nguvu ya Upanga na na hizo mbinu chafu za kusilimisha watu kiujanjajanja kama kuoa wanawake wa kikiristo na hata kutumia mapesa ya mafuta kuwahonga watu masikini.

mobile doctor said...

rudi shule ukasome ww yaan hata koran uwez usidanganye watu copy na paste ka ilivyo andikwa tafsir kama 4;3 na kadhalika koz kitabu cha koran hakina shaka ndan yake 2;2
ila kuna aya zizizo bayana na za mifano koran 3:7 sasa wajinga wasioamin utumia za mifano so soma vizur kijana na usipotoshe watu uislam haujaenea kwa jihad au vita
jihad katika uislam ni kuzuia mabaya na kuhamasisha mema tena mpaka makafiri wawaanze waislam katk din anayoilidhia mwenyez mungu na mitume waliopita kama nabii ibrahim, isihaka, yusufu,issa au yesu jina la kizungu,mtume muhamad, koran 3;19 sasa basi tumia akili din ya kiislam kwanza ni marufuku na hairuhusiwi mtu kulazimishwa kuslim au kusalim amri za mungu Allah pekeyake koran 109;6 sasa kivp jihad inaweza kueneza din ni kwa vile watoto, wazee, maskin, mayatima, wasiojiweza usaidiwa na waislam kama alivyoamrisha mwenye milk ya ulimwengu ambaye ana mtomto wala mshirika yaan Allah nasi kusema kuwa et kwa upanga . plse musidandie gar kwa mbele ninyi makafiri.

Unknown said...

Nimesoma uchambuzi wa ndugu Daniel Mwankemwa na comments zinazotolewa na watu mbali mbali hususani Waislamu. Linalonishangaza ni kwamba kwa upande wa Waislamu wanachokanusha kwamba Uislamu ulienea/unaenezwa kwa upanga ni nini? Je wanachokifanya leo Al Shabaab, Boko Haram, na ISIS kuua Wakristo na kuwalazimisha Wasilimu ni nini?

frozah said...

Halleluyah!! Muslims come tou Jesus

yesu ni mungu said...

waisilamu wote njooni kwa yesu.yeye anawapenda wote na ndiye mwokozi wa ulimwengu.wengi wenu wanatafsiri vibaya biblia.biblia ni kweli,ni neno la mungu aliyeziumba mbingu na nchi.ukiwa sio mkristo hakika hutaweza kuielewa biblia vizuri.ila kwa jina lenye uwezo na nguvu na mamlaka la yesu kristo mtaijua kweli.mungu awasaidie.sisi wakristo tunawapenda sana na hatupendi mzidi kupotea.tunazidi kuwaombea ndugu zetu

yesu ni mungu said...


Anonymous said...

Mtumishi hembu rejea vizuri maandiko yetu katika kurasa hii!!
Naona kama hayajajengwa na hoja zenye vigezo makini! Maana ya neno Uislam umelipatia kuwa ni Amani, sasa vp waipende vita?
Pia Ukisoma vizuri Quraan, na mafundisho mengine ya waislamu yanasema kuwa waislamu hawakumpiga adui pasipokuwa na uchokozi, na pia kabla ya kupigana pia walifikisha ujumbe wa busara, mwisho kabisa ndio walipigana,hivyo naona kama umewasingizia mtumishi, amri ya kupigana kwao ilikuja baada ya kuhakiki uchokozi na kutosalimu kwa adui,REJEA HISTORIA YA VITA YA WAAJEMI/WARUMI NA WAISLAMU wakiongozwa na Zaidi

Pia hikima ya waalimu wa kiislamu kushawishi kwa lugha safi na tamu kama ile ya watu wa jaula ndio imetushawishi kusilimu mtumishi, na si kama yule Mlokole anae piga kelele kama mwendawazimu pale posta,, yupo na mwingine anahutubia biblia kuwa imeruhusu pombe wakati hata kwa akili ya kawaida pombe inamadhara sana kimaadili!

uislamu nimeuona kuwa unazingatia saana maadili kuanzia tabia mpaka mavazi, kujisitiri kwa wanaume kutovaa vipensi na wanawake kwenda kumwabudu M.MUNGU na kichupi
? dah Unajua hata dem wangu wa kwanza zamani nilimchomolea Kanisani, yote ni kwa sababu nilipenda miguu yake, lakini kama angekuwa amejisitiri, nisingeshawishika....mbona masister wanavaa kama waislamu?
Afu maswali haya hata ukimuuliza Mchungaji huwa anatufukuzaga au anakwita pembeni,lakini pia hatujibu vizuri zaidi huwa anasema "mshaanza kuongopewa huko!"

Nina mengi lakini ngoja nimalize na maswali haya ya mwisho,

Vp mafundisho ya bilble yanatutaka kwa ujumla tuwe /turudi kundini napo tutakuwa salama, lakini cha ajabu uislamu ndio umebeba neno SALAM/AMANI, hapa inakuwa KRISTU lisinge tafsirika hivi?

Unknown said...

Anonymous Mtumishi. pole sana kwa sababu umesema umeingia kwenye Uislamu eti kwa kufikiri ni dini ya amani kwa maoni yangu umekosea sana. Kuna maswali magumu ambayo ukiulizwa kuhusu huo Uislamu, ninaamini utashindwa hata kujibu na mwisho utaishia kuleta shuku mbaya huku ukiukimbia ukweli. Mathalani unasema nini kuhusiana na aya hizi ndani ya Quran: 2:190, 5:15, 5:51, 6:151 na ufafanuzi wake, 9:30, 61:9 hiyo ndiyo amani uluyoiona wewe? Halafu linganisha na Yoh 14:27-28 ndani ya Biblia.

Masuala ya imani hupaswi kuyafuata kama kipofu tu, bali unatakiwa kuyafuata baada ya kujiridhisha na kuwa na hakika pasipo shaka. Kwako ISIS, DAESH, Boko Haram, Al Shabab, Muslim Brotherhood wanachokifanya ndiyo amani?

Anonymous said...

Daniel Mwankemwa
Hayo yote uliyoelezea ni Mbinu halisi za kutia Fitina baina ya Dini zilizokuwa zinaishi kwa amani nchini.Usiigize nchi za nje kuchafua nchi yako.Mola wetu ni mmoja
Waislamu pia wanazokashfa nyingi juu ya dini nyingine lakini hawapendi kushafua.
kwani Uislamu ni Imani yako hakuna anaemlazimisha mtu.

fatilia sana mihadhara ya dini ya Kiislamu Na Kikristo utajifunza mengi.

Anonymous said...

Upotofu gani aliowapoteza Marehemu Ahmed Deedat Allah amrehemu
yote aliyonakili yamo kwenye kitabu chenu Biblia.wewe vipi?kwahiyo unakiita kitabu chenu cha upotofu au sio?
naomba uhudhurie Mihadhara ya dini labda utaiona Haki.
Na ujumbe wa Qur ani tukufu.Mwenyezi ndie anaemuongoa ampendae.

Anonymous said...

2:190 inasema hivi "Na piganeni katika njia ya Mwenyezimungu na wale wanaokuoigeni, wala msianze uadui kwani mwenyezimungu hawapendi waanza uadui" hizo aya zinaendelea hadi 193 Lakini kwa kuwa wewe unaficha haki hukutaka kueleza.

5:14-15 inasema hivi:
"Na kutoka kwa wale waliosem:Sisi ni Wakristo tulichukuwa ahadi yao lakini wakasahaunsehemj ya waliyokumbushwa kwa hiyk tukaweka kti yao uadui na chuki mpaka siku ya kiyama na hapo mwenyezimungu atawaambia waliokuwa wakiyafanya" Enyi watu wa kitabu (Wayahudi na Wakristo) Amekwisha kujieni
mtume wetu anayekubainishieni mengi mliyokuwa mkiyaficha katika kitabu n anayesamehe mengi..."


6:151"Sema njooni nikusomeeni aliyokuharamishieni Mola wenu Mlezi... msimshirikishe na chochote, wazazi wafNyieni wema, msiwaue watoto wenu, msifanye mambo machafu kwa dhahiri au kwa siri wala msiue nafsi..."

Kwa kuwa unachuki umeshindwa kufikiri vizuri... MKIRISTO YEYOTE AKISOMA HIZO AYA ATASHAWISHIKA KUSILIMU, Hukutaka kunukuu matini ili kujifanya wajuuua.

Ama kuhusu Uchawi na Uganga umewasingizia waislamu, umeandika uongo! Katika Uislamu Mchawi yeyote amejitoa katika Uislamu na hukmu yake ni kifo, vili ndio iwe njia ya kuwaita watu waje ktk Uislamu!

Anonymous said...

pole sana kaka. mlani shetani maana hukusoma na kuelewa. vita vilivyo tajwa ni vya makafiri haikutajwa wakristo maana kurani hiyo hiyo inatambua kuna watu wanajiita wakristo na hao wakielezwa ukweli maana ni watu wa vitabu wata silimu. lakini kwavile wewe ni kafiri hutaki hata wakristo kwa mujibu wa bibilia na qurani wapate uongofu. jee hukujua yakua yesu alisema hakuleta amani hapa duniani alileta upanga? soma uelewe usiwe zuzu. asanteni.

Unknown said...

ubarikiwe Mtumishi wa Mungu. kazi yako ni njema

Anonymous said...

Mbona Ukweli hamuutaki?KIla goti litaadhibiwa kwa kosa lake.Vipi Yesu aje kuchukua dhambi za wengine.na yeye kama munavyoamini kuwa ni Mungu ,Mungu gani anachukua dhambi za watu wake? Sio kuwasamehe ni kubeba dhambi zao? Kuweni na kufikiri sio kuamini tu kila munaloambiwa

Anonymous said...

Mr Daniel ukitaka kufahamu ukweli chukua agano la kele na jipya kabla ya kuanza kusoma weka jina yesu katika kila sehemu anayosema mungu,bwana,yohova,elai nk au utwajwa wowote unaoamanisha m/mungu au mungu mlezi hapo ukweli utaona kama mungu awezi leo kua mtoto kesho baba au leo hivi kesho vile mungu ni wa milele hakuna kubadilika badilika kama kinyonga

Unknown said...

Hawa waislam ndio waanzilishi wa ugaidi ulimwenguni kwa kisingizio cha kueneza dini

Anonymous said...

Wewe John Sombi,usidanganyike hakuna anaelazimishwa kuingia Dini ya Kiislam.Hayo unayosema Magaidi ni vitisho vya kuwafanya watu waogope Dini Ya Mwenye ezi Mungu.Dini ya Kiislamu.eleza wapi Uislamu uliingizwa kwa vita.Mnatishwa ili mawazo yenu yabaki kuuchukia Uislamu.Kwanini Mchungaji akiingia dini ya haki ya kiislamu ananyanganywa Nyumba,gari na anabaniwa matumizi?Jibu aone maisha magumu akubali kupotezwa.

Anonymous said...

Waliowauwa mitume na Manabii ni waislamu?Naomba jibu

Unknown said...

Maasha Allah!!.. so true, very true ikhuwan.

Unknown said...

Hahahaha....Kamuombee Yusuph Estes wa Marekani...na Nicolas Anelka...na wengine waliosilimu...ama si mwasema Jina la Yesu ni kila kitu, piga maombi hapohapo ulipo warudie ukristo

Unknown said...

Ndio maana tunasema nyie huwa mnatwikwa imani na mnaamini 100% na kichwa na miguu bila kutumia akili!.. LEO WATU WENYE AKILI WANAJUA ISIS NI ISRAEL NA WAMAREKANI...HAYO.MAKUNDI YA KIGAIDI YOTE NI WAO WANAYAANZISHA KWA AJILI YA ULAFI WAO NA KUWASHIKA MASIKIO NYIE KONDOO MSOTUMIA AKILI..MNAAMINI TU....SOMA, TAFUTA DOCUMENTARIES, KISHA PAMBANUA.

Unknown said...

Mwenyezi Mungu azidi kukupa nuru ktk maisha yako.

Anonymous said...

Mtu mwenye akili timamu za kawaida HAPATI SHIDA kulinganisha kuamini kuwa Mkristo tokana na hali ya kiimani duniani ukiulinganisha Uislamu na Ukristo! Nani adanganyike na Usilamu ambao umechafua amani ya dunia, isitoshe mifano midogomidogo watu wamekutwa na majambia misikitini ukiacha hayo ya Ugaidi? Kunyamaza kwetu wakristo si kuwa hatuna hoja ni malezi yetu! Nyie SI wapiga kelele kudai ubwabwa ambao hauwastahili? Mara oo "tunanyanyaswa"! Ukweli upo hapo hapo, YESU alikuwapo kwanza kabla ya huyo wa kwenu....ambaye jina lake haliwezi hata kuponya mgonjwa!

Dini gani yenye jazba! Mkikwaruzwa kidogo tu ni shida! Ndo maana huko Uarabuni hapakaliki!

Soma Mathayo 6:14-15 Sisi tumefundishwa " Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao, Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi. Bali msipowasamehe watu makosa yao, wala Baba yenu (Mungu) hatawasamehe ninyi makosa yenu". Yanayoendelea huko Arabuni ni kwasababu ya mafundisho yenu ya visasi.

Unknown said...

kwanza uislamu haukuenea kawa upanga umeenea kwa dawaah au kulingania watu, pia baada ya mateso makali kuyapata mtume sasa mungu akaamuamrisha mtume panga itumike ili kupata haki. lakini pia sijaona point zako ila ni uzushi na mungu kakuumbua kwasababu huna point na hakuna aliyeelewa.... HEBU SILIMU NA KUWA MUISLAMU KAMA UNATAK KUUONA UFALME WA MUNGU

Anonymous said...

Waliowauwa mitume na Manabii ni waislamu?Naomba jibu
sijapata jibu
Hawa jamaa wanataka kuingangusha dini ya haki.fitina zao.chuki zao na vishawishi vyao kwa watu wenye Imani ndogo kwa Allah ndio wanaokubaliana nao.
hata mukiwaambia lolote ndani ya nyoyo zao kumeingia Maradhi ya kumchukia Allah hawatabadilika kamwe.
sawa sawa na kumpigia mbuzi gitaa.

Unknown said...

inaonekana huyo mkristo ana jinn sugu,,kwa imani yake yesu ni mwana wamungu,na marym atamwitaje mungu,sub'hanallah ametakasika mwenyenzi mungu, ambaye hana mshirika,,mungu hana mwana wala mke wala mjukuu wala hanashida navyo: milima karibu itapasuka kwa kumsingizia mungu kuana mwana,

Unknown said...

waislamu Hata mfanyeje hamuwezi kamwe kulishinda taifa la Bwana la Israel .iyo imetamkwa na Mwenyezi mungu

Anonymous said...

wewe Casto Aloyce waislamu hatuna mashindano ya mpira .ila tunataka kuifata haki ambayo wewe na wenzio hamtaki kuifata.Taifa la israel sio dini ni Taifa.
uislamu sio Taifa wala Kabila ni Dini Ya Haki.halafu toa hiyo Aya aliosema Mwenyeezi Mungu hamuutaishinda taifa la Israel.

Wingu La Mashahidi said...

Je! unafahamu kuwa Eliya ameshakuja kama BWANA alivyoahidi katika malaki 4:4-6, angekuja kabla ya kuja kwa ile siku ya kuogofya ya BWANA, Mungu alimtuma mjumbe wake WILLIAM BRANHAM, katika kizazi chetu kuturudisha sisi katika ukristo wa biblia, ishara na miujiza ya kupita kawaida iliambatana naye katika huduma yake, BWANA YESU alitembea naye kwa namna ya kipekee ambayo haijatokea hata katika historia ya kizazi chetu. je! unaufahamu ujumbe Mungu aliompa kuuleta?? Fuatilia ujue zaidi, tunaishi katika nyakati ambayo BWANA YESU KRISTO yupo mlangoni kurudi. Mungu akubariki.
http://wingulamashahidiwakristo.blogspot.com/2016/09/mahojiana-ya-ndugu-william-branham_78.html#links

Unknown said...

Naona mnapoteza muda kujadili ualali wa dini flan..mfano waislam eti mnadai kitabu chenu kilishushwa kutoka mbinguni sasa najiuliza nani alikipokea wapi,muda gani na kwastaili gani alikidaka au kilidondoka? Huyo sijui jamaa yenu muhamad kwanini alirogwa kwa muda wa mwakamzima km ni mtu wa mungu kupitia vitabu vyenu vya hadithi. Kwanini muhamad aoe katoto kenye miaka6 alafu akagonge akiwa na miaka9 nayeye akiwa na miaka59 hivi ingekuwa hapa bongoleo siangekula miaka30 ya ubakaji, kwanini awafundishe mke na mume jinsi ya kuhondomola eti dhambi zitaisha kupitia vidole au kutawaza kupitia udongo tena ktk sehemu za siri km wamekosa maji baada ya kuhondo sasa kibiolojia siuchafu huo tena kwa demu atapata UTI. Kwanini muhamad awafundishe hadi mikao wa kula chakula kwani mungu hakuwapa akili? Kwanini awafundishe kuua binadamu wenzenu kwa mawe mkifumaniana hata km iyotabia ilikuwepo zaman kwann abariki wakati yesu alilipinga hilo, hivi kisheria sikosa la jinai ndugu zangu? Yesu hakusoma lakini alijua kusoma na kuandika je kwann mohamad hakujua kusoma wakati alikuja miaka577 baada ya kristo tena maendeleo ya kiteknolojia yalishasonga mbele na chaajabu mitume yote ilijua kusoma kasoro msela wenu mnaomuita mtume muhamad. Kuhusu tamaa zake za kuoa wake wengi nahata waliomzidi umri nazipotezea hazinihusu nistarehe yake ila nawaonea huruma mnavyopelekana chaka kama muhamad alivyo wachezea mchezo huku akijua ukweli ulivyo mfano alivyo andika kitabu chenu cha kuwapotosha mnakiita sijui kuruani alichokiandika kwa chabo ya biblia na kupunguza na kuongeza yake mfano eti yesu alisema mm naondoka ila atakuja mtu wa mwisho wakati ktk bible anamaanisha roho mtakatifu ila muhamad akajiandika jina lake. Leo hii mnalilia mahakama ya kadhi ili mzidi kuumizana huku mkiamini muhamad alikuja kuketa umoja kumbe alikuja(alianza)kuleta migogoro kwa kutumia vita vya upanga wa chuma na hapo msidanganywe na upanga aliousema yesu wenyemaana ya injili inayomkata shetani vikali...tatizo waislamu wanamisimamo kuliko uelewa wanadanganyana kwakutumia mifano ya kimwili huku wakristo walielimishwa kupitia mifano ya kiroho ambayo ndiyo njia pekee ya kuingia ktk mbingu ya mwenyezi mungu...leo hii utasikia wakiuliza tuambie ukristo umeandikwa wapi kuwa ni dini? Lakini hawajiulizi nini maana ya neno kristo(christian) lilitokea wapi, kwanini yesu anaitwa yesu christo it means maanayake ni yesu mwokozi,so jibu rahisi ukristo ulianza mala tu yesu alipozaliwa kimwili na kuanza kufundisha watu wakaelimika wakawa manabii wa christo yesu basi na imani hiyo iliyozaliwa kupitia elimu aliyoiambukiza jesus tukaibatiza ukristo. Cha ajabu sheria 10 za mwenyezi mungu baadhi hupingana na sheria alizozibuni/kuzienzi muhamad kama kuua mtu kwa kupigwa mawe,kuoa binti chini ya miaka18 n.k.....dah nduguzetu mnatia huruma na sitashangaa nikitukanwa kwa thread hii maana wenzetu kwa kujilipua hamjambo mfano mdogo mtoto alikojolea msahafu wenu basi nchinzima maandamano yani hatatu kujiuliza yule simtoto tu hajui kitu. Ila nashukuru msahafu umeandikwa kiarabu mnachokisingizia kuruani maana watoto wanakalilitu hawaelewi kilichoandikwa maana wakijua kilakitu watapakimbia. Huu mchezo hautaki hasira..good day

Unknown said...

Yesu alipewa utume na binadamu wa kikristo na kitabu chake ni biblia na Nabii issa (a.s) alipewa injili tukufu

Anonymous said...

Mbona comment nyingine hampost au zinawagusa? musiwe wabaguzi toeni zote zinazoandikwa.
narudia kumjibu casto Aloyce
Uislamu sio taifa ni Dini ya Mwenyeezi Mungu muulize askofu wako mkuu wa duniani aliesoma atakujibu,usiulize wanaolipwa hela kuharibu dini bila elimu ya kutosha.
toa Aya ya mwenyeezi Mungu iliyosema taifa la Israel halitashindwa.usimsingizia Mwenyeezi Mungu Utaadhibiwa.
Anaefata ukristo amefata taifa la Israel sio dini au vipi Casto?

Imani ongara said...

Jesus is my everything

Imani ongara said...

Yesu ni mwokozi wa ulimwenguni

 
Powered by Blogger